Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:27-46 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:27-46 in Biblia ya Kiswahili

27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili