Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:26-34 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:26-34 in Biblia ya Kiswahili

26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili