26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.