Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 78:12-20 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 78:12-20 in Biblia ya Kiswahili

12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Zaburi 78 in Biblia ya Kiswahili