Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 74:4-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 74:4-11 in Biblia ya Kiswahili

4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Zaburi 74 in Biblia ya Kiswahili