Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 72:7-14 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 72:7-14 in Biblia ya Kiswahili

7 Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8 Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9 Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10 Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11 Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12 Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13 Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
14 Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
Zaburi 72 in Biblia ya Kiswahili