Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 69:25-34 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 69:25-34 in Biblia ya Kiswahili

25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
Zaburi 69 in Biblia ya Kiswahili