Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 63:3-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 63:3-10 in Biblia ya Kiswahili

3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Zaburi 63 in Biblia ya Kiswahili