Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 55:6-14 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 55:6-14 in Biblia ya Kiswahili

6 Nikasema, “Oh, kama tu ningekuwa na mabawa kama njiwa! Ningelipaa mbali na kupata pumziko.
7 Tazama, ningeenda mbali; ningekaa jangwani. Selah
8 Ningefanya haraka kuja mafichoni mwako kuzikimbia dhoruba na tufani.”
9 Uwaangamize, Bwana, vuruga lugha zao! Kwa maana nimeona vurugu na ugomvi katika mji.
10 Mchana na usiku wao huenda kwenye kuta zake; uchafu na ufisadi uko katikati yake.
11 Uovu uko katikati yake; ukandamizaji na uongo hauiachi mitaa yake.
12 Kwa maana hakuwa adui aliye nikemea, hivyo ningevumilia; wala ingekuwa ni yule aliye nichukia aliyejiinua mwenyewe dhidi yagu, hivyo ningejificha asinione.
13 Lakini ulikuwa wewe, mtu sawa na mimi, mwenzangu na rafiki yangu.
14 Tulikuwa na ushirika mtamu pamoja; tuliingia katika nyumba ya Mungu tukiwa na umati mkubwa.
Zaburi 55 in Biblia ya Kiswahili