Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 51:4-16 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 51:4-16 in Biblia ya Kiswahili

4 Dhidi yako, wewe pekee, nimetenda dhambi na kufanya uovu mbele ya macho yako; uko sawa usemapo; wewe uko sahahi utoapo hukumu.
5 Tazama, nilizaliwa katika uovu; pindi tu mama yangu aliponibeba mimba, nilikuwa katika dhambi. Tazama, wewe unahitaji uaminifu ndani ya moyo wangu;
6 katika moyo wangu wewe utanifanya niijue hekima.
7 Unisafishe kwa hisopo, nami nitakuwa safi; unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 Unifanye kusikia furaha na shangwe ili kwamba mifupa ulioivunja ifurahi.
9 Uufiche uso wako mbali na dhambi zangu na uyafute maovu yangu yote.
10 Uniumbie moyo safi, Mungu, na uifanye upya roho ya haki ndani yangu.
11 Usiniondoe uweponi mwako, na usimuondoe roho Mtakatifu ndani yangu.
12 Unirudishie furaha ya wokovu wako, na unihifadhi mimi kwa roho ya utayari.
13 Ndipo nitawafundisha wakosaji jia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
14 Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
15 Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
16 Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
Zaburi 51 in Biblia ya Kiswahili