Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 50:2-9 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 50:2-9 in Biblia ya Kiswahili

2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
Zaburi 50 in Biblia ya Kiswahili