Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 50:2-11 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 50:2-11 in Biblia ya Kiswahili

2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
Zaburi 50 in Biblia ya Kiswahili