16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.