Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 44:11-23 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 44:11-23 in Biblia ya Kiswahili

11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa,...
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Zaburi 44 in Biblia ya Kiswahili