7 Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
8 Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
9 Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
10 Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
11 Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
12 Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
13 Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.