16 Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
17 Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
18 Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
19 Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
20 Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
21 Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.