4 Kisha ufurahi mwenyewe katika Yahwe, naye atakupa matamanio ya moyo wako.
5 Umkabidhi njia zako Yahwe; uamini katika yeye, naye atatenda kwa niaba yako.
6 Yeye ataidhihilisha haki yako kama mchana na usafi wako kama mwangaza wa mchana.
7 Uwe kumya mbele za Yahwe na umsubiri yeye kwa uvumilivu. Usikasirike ikiwa kuna mtu anafanikiwa kwa kile afanyacho, au afanyapo njama za uovu.
8 Usikasilile na kugadhabika. Usiogope. Hii huleta matatizo tu.
9 Watendao maovu watafutiliwa mbali, bali wale wamngojao Yahwe watairithi nchi.