27 Acha uovu na ufanye yaliyo mema; ndipo utakapokuwa salama milele.
28 Kwa maana Yahwe hupenda haki naye hawaachi wafuasi waaminifu. Wao hutunzwa milele, lakini uzao wa waovu utafutiliwa mabli.
29 Wenye haki watairithi nchi na kuaa huko milele.
30 Mdomo wa mwenye haki huongea hekima na huongeza haki.
31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; miguu yake haitelezi.
32 Mtu mwovu humvizia mwenye haki na kutafuta kumuua.
33 Yahwe hatamuacha yeye kwenye mkono wa mtu mwovu wala kumlaumu atakapohukumiwa.
34 Umngoje Yahwe na uishike njia yake, naye atakuinua uimiliki nchi. Atakapo waondosha waovu wewe utaona.
35 Nimewaona waovu na mtu wa kutisha akienea kama mti wa kijani katika udongo wa asili.
36 Lakini nilipopita tana mara nyingine, hakuwepo pale. nilimtafuta, lakini sikumpata.
37 Uwachunguze watu waadilifu, na uwatambue wenye haki; kuna hatima nzuri kwa ajili ya mtu wa amani.