Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 35:8-19 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 35:8-19 in Biblia ya Kiswahili

8 Uharibifu na uwapate wao kwa kushitukiza. Mtego ambao wameutega na uwanase wao. Na wadumbukie humo, ili kwamba waangamizwe.
9 Bali mimi nitakuwa nafuraha ndani ya Yahwe na ndani ya wokovu wake.
10 Mifupa yangu yote itasema, “Yahwe, ni nani kama wewe, uokoaye walio onewa mkononi mwa walio na nguvu kuwazidi wao na masikini na wahitaji mkononi mwa wale wanaojaribu kuwaibia?”
11 Mashahidi wa uongo wamesimama; wananishitakia uongo.
12 Kwa ajili ya wema wananilipa mabaya. Nina huzuni nyingi.
13 Lakini, walipokuwa akiugua, nilivaa magunia; nilifunga kwa ajili yao huku kichwa changu kikiinamia kifuani kwangu.
14 Nilienenda katika huzuni kana kwamba walikuwa ni ndugu zangu; niliinama chini nikiomboleza kana kwamba ni kwa ajili ya mama yangu.
15 Bali mimi nilipokuwa mashakani, walifurahi sana na kukutanika pamoja; walikutanika pamoja kinyume na mimi, nami nilishangazwa nao. Walinirarua bila kuacha.
16 Kwa dharau kabisa walinidhihaki; walinisagia meno yao.
17 Bwana, mpaka lini utaendelea kutazama? uiokoe roho yangu na mashambulizi yao ya maagamizi uyaokoe maisha yangu na simba.
18 Nami nitakushukuru wewe katika kusanyiko kubwa; nitakusifu kati ya watu wengi.
19 Usiwaache maadui zangu wadanganyifu kufurahi juu yangu; usiwaache waendelee na mipango yao ya uovu.
Zaburi 35 in Biblia ya Kiswahili