Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 33:3-16 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 33:3-16 in Biblia ya Kiswahili

3 Mwimbieni yeye wimbo mpaya; pigeni kwa ustadi na muimbe kwa furaha.
4 Kwa kuwa maneno ya Mungu ni ya hakika, na kila afanyacho ni haki.
5 Yeye hupenda haki na kutenda kwa haki. Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe.
6 Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa, na nyota zote ziliumbwa kwa pumzi ya mdomo wake.
7 Yeye huyakusanya maji ya baharini kama rundo; naye huiweka bahari katika ghala.
8 Basi ulimwengu wote umwogope Yahwe; wenyeji wote wa ulimwengu wamuhofu yeye.
9 Kwa maana yeye alisema, na ikafanyika; aliamuru, na ikasimama mahali pake.
10 Yahwe huvunja muungano wa mataifa; naye huishinda mipango ya wanadamu.
11 Mipango ya Yahwe husimama milele, mipango ya moyo wake ni kwa ajili ya vizazi vyote.
12 Limebarikiwa taifa ambalo Mungu wao ni Yahwe, watu ambao yeye amewachagua kama warithi wake.
13 Yahwe anatazama kutoka mbinguni; yeye huona watu wote.
14 Kutokea mahali ambapo yeye anaishi, huwatazama wote waishio juu ya nchi.
15 Yeye anaye iumba mioyo yao na kuyaona matendo yao yote.
16 Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa; shujaa haokolewi na nguvu zake nyingi.
Zaburi 33 in Biblia ya Kiswahili