1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,