Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 29:3-9 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 29:3-9 in Biblia ya Kiswahili

3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
Zaburi 29 in Biblia ya Kiswahili