Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 25:9-16 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 25:9-16 in Biblia ya Kiswahili

9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Zaburi 25 in Biblia ya Kiswahili