12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!