4 Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa.
6 dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
7 Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
8 Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
9 Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10 Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
11 Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
12 Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13 Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.