Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 18:4-10 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 18:4-10 in Biblia ya Kiswahili

4 Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa.
6 dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
7 Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
8 Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
9 Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10 Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
Zaburi 18 in Biblia ya Kiswahili