2 Yahwe huijenga tena Yerusalemu, huwakusanya pamoja watu wa Israeli waliotawanyika.
3 Huponya mioyo iliyopondeka na kuganga majeraha yao.
4 Huzihesabu nyota, naye huzipa majina zote.
5 Ukuu ni wa Bwana wetu na nguvu zake ni za kutisha, ufahamu wake hauwezi kupimika.
6 Yahwe huwainua wanyonge, huwashusha chini wenye jeuri.
7 Mwimbieni Yahwe kwa shukurani, mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi.