9 Yahwe ni mwema kwa wote; huruma zake zi juu ya kazi zake zote.
10 Vyote ulivyo viumba vitakushukuru wewe, Yahwe; waaminifu wako watakutukuza wewe.
11 Waaminifu wako watanena juu ya utukufu wa ufalme wako, na watahubiri juu ya nguvu zako.
12 Watayafanya matendo makuu ya Mungu ya julikane na wanadamu na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
13 Ufalme wako ni wa milele, na mamlaka yako ya dumu kizazi hata kizazi.
14 Yahwe huwategemeza wote waangukao na huwainua wote walioinama chini.