Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 145:13-21 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 145:13-21 in Biblia ya Kiswahili

13 Ufalme wako ni wa milele, na mamlaka yako ya dumu kizazi hata kizazi.
14 Yahwe huwategemeza wote waangukao na huwainua wote walioinama chini.
15 Macho ya wote yanakungoja wewe; nawe huwapa chakula chao kwa wakati sahihi.
16 Huufungua mkono wako na hukidhi haja ya kila kiumbe hai.
17 Yahwe ni mwenye haki katika njia zake zote na neema katika yote afanyayo.
18 Yahwe yu karibu na wote wamwitao, wale wamwitao yeye katika uaminifu.
19 Hutimiza haja za wale wanao mheshimu yeye; husikia kilio chao na kuwaokoa.
20 Yahwe huwalinda wale wampendao, lakini atawaangamiza waovu wote.
21 Kinywa changu kitazinena sifa za Yahwe; wanadamu wote na walitukuze jina lake takatifu milele na milele.
Zaburi 145 in Biblia ya Kiswahili