Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 144:1-6 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 144:1-6 in Biblia ya Kiswahili

1 Atukuzwe Yahwe, mwamba wangu, anifundishaye mikono yangu vita na vidole vyangu kupigana.
2 Wewe ni uaminifu wa agano langu na ngome yangu, mnara wangu mrefu na uniokoaye, ngao yangu na yule ambaye katika yeye napata kimbilio, uyatiishaye mataifa chini yangu.
3 Ee Yahwe, mtu ni kitu gani hata umtazame au mwana wa mtu hata umfikirie?
4 Mtu ni kama pumzi, siku zake ni kama uvuli upitao.
5 Ee Yahwe uziinamishe mbingu na ushuke chini, uiguse milima na uifanye kutoa moshi.
6 Utume umeme uwatawanye adui zangu; upige mishale yako na uwavuruge.
Zaburi 144 in Biblia ya Kiswahili