1 Yahwe, uniokoe dhidi ya waovu; unikinge dhidi ya watu wenye vurugu.
2 Wao wanapanga uovu mioyoni mwao; wanasababisha mapigano kila siku.
3 Ndimi zao zinajeruhi kama nyoka; sumu ya fira imo midomoni mwao. Selah
4 Ee Yahwe, unilinde dhidi ya mikono ya waovu; unikinge na vurugu za watu wanaopanga kuniangusha.
5 Wenye majivuno wameweka mtego kwa ajili yangu; wameeneza nyavu; wameweka kitanzi kwa ajili yangu. Selah
6 Nilimwambia Yahwe, “Wewe ni Mungu wangu; usikie kilio changu unihurumie.”
7 Ee Yahwe, Bwana wangu, wewe ni mwenye nguvu uwezaye kuniokoa; hunifunika ngao kichwa changu siku ya vita.