Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 132:10-18 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 132:10-18 in Biblia ya Kiswahili

10 Kwa ajili ya mtumishi wako Daudi, usimuache mfalme wako uliye mpaka mafuta.
11 Yahwe alimwapia Daudi kiapo cha uhakika, kiapo cha uhakika ambacho hatakivunja: “Nitamuweka mmoja wa wazawa wako kwenye kiti chako cha enzi.
12 Kama wana wako watalishika agano langu na sheria ambazo nitawafundisha, watoto wao pia watakaa kwenye kiti chako cha enzi milele.”
13 Hakika Yahwe ameichagua Sayuni, ameitamani kwa ajili ya makao yake.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele. Nitaishi hapa, kwa kuwa ninapatamani.
15 Nitapabariki sana kwa mahitaji. Nitawatosheleza maskini wake kwa mkate.
16 Nitawavisha makuhani wake kwa wokovu, waaminifu wake watashangilia kwa furaha.
17 Hapo nitachipusha pembe kwa ajili ya Daudi na kuweka taa juu kwa ajili ya mpakwa mafuta wangu.
18 Nitawavisha adui kwa aibu, bali juu yake taji yake itang'aa.”
Zaburi 132 in Biblia ya Kiswahili