98 Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.
99 Ninauelewa zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa maana ninazitafakari amri za agano lako.
100 Ninaelewa kuliko wale wanaonizidi umri; hii ni kwa sababu nimeyashika maagizo yako.
101 Nimeiepusha miguu yangu na kila njia ya uovu ili niweze kulitii neno lako.
102 Sijaenda kinyume na amri zako za haki, kwa maana wewe umenifundisha.