86 Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
87 karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.
88 Kwa upendo wako thabiti, uniweke hai, ili niweze kuzitii amri zako. LAMEDH.
89 Yahwe, neno lako linasimama milele; neno lako limefanywa imara mbinguni.
90 Uaminifu wako wadumu kwa ajili ya vizazi vyote; umeiimarisha nchi, nayo inadumu.
91 Vitu yote yaliendelea mpaka leo hii, kama vile ulivyosema katika amri zako za haki, maana vitu vyote ni watumishi wako.
92 Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningeangamia katika mateso yangu.
93 Sitayasahau kamwe maagizo yako, maana kupitia hayo umeniweka hai.
94 Mimi ni wako, kwa maana ninayatafuta maagizo yao.
95 Waovu hujiandaa kuniangamiza, lakini nitatafuta kuzielewa amri za agano lako.
96 Nimeona kuwa kila kitu kina mipaka, lakini amri zako ni pana, zaidi ya mipaka. MEM.
97 Oh ni jinsi gani naipenda sheria yako! Ni tafakari yangu mchana kutwa.
98 Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.