77 Unihurumie ili niweze kuishi, kwa maana sheria yako ni furaha yangu.
78 Wenye kiburi na waaibishwe, maana wamenitukana; bali mimi nitayatafakari maagizo yako.
79 Wale wote wanao kucha wewe na wanigeukie, wale wazijuao amri za agano lako.
80 Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
81 Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
82 Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
83 Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
84 Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
85 Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
86 Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
87 karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.