Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:73-90 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:73-90 in Biblia ya Kiswahili

73 Mikono yako imeniumba na kunitengeneza; unipe uelewa ili niweze kujifunza amri zako.
74 Wale wanao kucha wewe watafurahi wanionapo kwa sababu ninapata tumaini katika neno lako.
75 Ninajua, Yahwe, kuwa amri zako ni za haki, na kuwa katika uaminifu ulinitesa.
76 Agano lako aminifu na linifariji, kama ulivyomwahidi mtumishi wako.
77 Unihurumie ili niweze kuishi, kwa maana sheria yako ni furaha yangu.
78 Wenye kiburi na waaibishwe, maana wamenitukana; bali mimi nitayatafakari maagizo yako.
79 Wale wote wanao kucha wewe na wanigeukie, wale wazijuao amri za agano lako.
80 Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
81 Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
82 Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
83 Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
84 Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
85 Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
86 Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
87 karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.
88 Kwa upendo wako thabiti, uniweke hai, ili niweze kuzitii amri zako. LAMEDH.
89 Yahwe, neno lako linasimama milele; neno lako limefanywa imara mbinguni.
90 Uaminifu wako wadumu kwa ajili ya vizazi vyote; umeiimarisha nchi, nayo inadumu.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili