Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:67-75 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:67-75 in Biblia ya Kiswahili

67 Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
68 Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.
69 Wenye kiburi wamenichafua kwa uongo, lakini niliyashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.
70 Mioyo yao ni migumu, lakini ninafurahia katika sheria yako.
71 Ni vizuri kwangu kuwa nimeteseka ili niweze kujifunza sheria zako.
72 Maagizo yatokayo kinywani mwako ni ya thamani zaidi kwangu kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha. YOD.
73 Mikono yako imeniumba na kunitengeneza; unipe uelewa ili niweze kujifunza amri zako.
74 Wale wanao kucha wewe watafurahi wanionapo kwa sababu ninapata tumaini katika neno lako.
75 Ninajua, Yahwe, kuwa amri zako ni za haki, na kuwa katika uaminifu ulinitesa.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili