65 Wewe umemtendea mema mtumishi wako, Yahwe, sawasawa na neno lako.
66 Unifundishe utambuzi sahihi na uelewa, kwa kuwa nimeamini katika amri zako.
67 Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
68 Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.