56 Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
57 Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
58 Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
59 Nilizichunguza njia zangu na kugeuzia miguu yangu kwenye amri za agano lako.
60 Naharakisha na sichelewi kuzishika amri zako.
61 Kamba za waovu zimenifunga; nami sijaisahau sheria yako.
62 Katikati ya usiku ninaamka kukushukuru wewe kwa sababu ya amri za haki yako.
63 Ninaurafiki na wale wanao kuabudu wewe, wale wote watiio maagizo yako.
64 Yahwe, nchi, imejaa uaminifu wa agano lako; unifundishe sheria zako. TETH.
65 Wewe umemtendea mema mtumishi wako, Yahwe, sawasawa na neno lako.
66 Unifundishe utambuzi sahihi na uelewa, kwa kuwa nimeamini katika amri zako.
67 Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
68 Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.