Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:46-58 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:46-58 in Biblia ya Kiswahili

46 Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
47 Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.
48 Nitaziinulia mikono yangu amri zako, nizipendazo; nitazitafakari sheria zako. ZAYIN.
49 Kumbuka ahadi yako kwa mtumishi wako kwa sababu umenipa tumaini.
50 Hii ni faraja yangu katika mateso: kuwa ahadi yako imeniweka hai.
51 Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
52 Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
53 Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.
54 Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu katika nyumba ninayoishi kwa muda.
55 Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
56 Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
57 Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
58 Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili