42 ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
43 Usiliondoe neno la kweli mdomoni mwangu, maana nimesubiri kwa ajili ya amri zako za haki.
44 Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.
45 Nitaenenda salama, maana ninayatafuta maagizo yako.
46 Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
47 Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.