Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:166-175 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:166-175 in Biblia ya Kiswahili

166 Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167 Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168 Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169 Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
170 Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
171 Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, maana amri zako zote ni za haki.
173 Mkono wako unisaidie, maana nimechagua maagizo yako.
174 Ninautamani wokovu wako, Yahwe, na sheria yako ni furaha yangu.
175 Naomba niishi na nikusifu wewe, na amri zako za haki zinisaidie.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili