163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165 Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166 Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167 Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168 Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169 Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
170 Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.