Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:158-171 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:158-171 in Biblia ya Kiswahili

158 Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
159 Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160 Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161 Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
162 Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165 Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166 Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167 Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168 Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169 Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
170 Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
171 Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili