Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:156-163 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:156-163 in Biblia ya Kiswahili

156 Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
157 Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
158 Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
159 Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160 Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161 Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
162 Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili