Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:147-153 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:147-153 in Biblia ya Kiswahili

147 NInaamka asubuhi kabla jua halijachomoza na kulia kwa ajili ya msaada.
148 Ninatumaini katika maneno yako. Macho yangu yako wazi usiku kucha ili niweze kutafakari juu ya neno lako.
149 Sikia sauti yangu katika uaminifu wa agano lako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika amri zako za haki.
150 Wale wanaonitesa wananikaribia, lakini wako mbali na sheria yako.
151 Wewe uko karibu, Yahwe, na amri zako ni za kuaminika.
152 Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
153 Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili