Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:146-165 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:146-165 in Biblia ya Kiswahili

146 Ninakuita wewe; uniokoe, nami nitazitii amri za agano lako.”
147 NInaamka asubuhi kabla jua halijachomoza na kulia kwa ajili ya msaada.
148 Ninatumaini katika maneno yako. Macho yangu yako wazi usiku kucha ili niweze kutafakari juu ya neno lako.
149 Sikia sauti yangu katika uaminifu wa agano lako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika amri zako za haki.
150 Wale wanaonitesa wananikaribia, lakini wako mbali na sheria yako.
151 Wewe uko karibu, Yahwe, na amri zako ni za kuaminika.
152 Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
153 Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
154 Unitetee na kunikomboa; unihifadhi, kama ulivyo ahidi katika neno lako.
155 Wokovu uko mbali na waovu, maana hawazipendi amri zako.
156 Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
157 Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
158 Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
159 Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160 Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161 Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
162 Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165 Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili