Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:136-176 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:136-176 in Biblia ya Kiswahili

136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
138 Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
139 Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
140 Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
141 Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.
142 Hukumu yako ni ya haki milele, na sheria yako ni ya kuaminika.
143 Japo dhiki na taabu vimenipata, amri zako bado ni furaha yangu.
144 Amri za agano lako ni za haki milele; unipe uelewa ili niweze kuishi. QOPH.
145 Nililia kwa moyo wangu wote, “Unijibu, Yahwe, nitazishika sheria zako.
146 Ninakuita wewe; uniokoe, nami nitazitii amri za agano lako.”
147 NInaamka asubuhi kabla jua halijachomoza na kulia kwa ajili ya msaada.
148 Ninatumaini katika maneno yako. Macho yangu yako wazi usiku kucha ili niweze kutafakari juu ya neno lako.
149 Sikia sauti yangu katika uaminifu wa agano lako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika amri zako za haki.
150 Wale wanaonitesa wananikaribia, lakini wako mbali na sheria yako.
151 Wewe uko karibu, Yahwe, na amri zako ni za kuaminika.
152 Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
153 Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
154 Unitetee na kunikomboa; unihifadhi, kama ulivyo ahidi katika neno lako.
155 Wokovu uko mbali na waovu, maana hawazipendi amri zako.
156 Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
157 Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
158 Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
159 Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160 Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161 Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
162 Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165 Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166 Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167 Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168 Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169 Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
170 Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
171 Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, maana amri zako zote ni za haki.
173 Mkono wako unisaidie, maana nimechagua maagizo yako.
174 Ninautamani wokovu wako, Yahwe, na sheria yako ni furaha yangu.
175 Naomba niishi na nikusifu wewe, na amri zako za haki zinisaidie.
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; mtafute mtumishi wako, kwa maana sijazisahau amri zako.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili