Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:133-143 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:133-143 in Biblia ya Kiswahili

133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
135 Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
138 Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
139 Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
140 Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
141 Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.
142 Hukumu yako ni ya haki milele, na sheria yako ni ya kuaminika.
143 Japo dhiki na taabu vimenipata, amri zako bado ni furaha yangu.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili