Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 119:129-137 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 119:129-137 in Biblia ya Kiswahili

129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
135 Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
Zaburi 119 in Biblia ya Kiswahili